Timu ya soka ya URA ya Uganda jana ilianza vyema michuano ya Kombe la Tusker baada ya kuilaza Mtibwa Sugar 1-0 katika mechi ya fungua dimba iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini, Dar es Salaam.
Bao la URA lilizamishwa na Tony Maweje katika dakika ya 50, ambaye alipokea pasi kutoka kwa Eric Obua katika mchezo huo wa kundi A.
Leo mashindano hayo yanatazamiwa kuendelea kwa kuzikutanisha Tusker FC ya Kenya na Prisons ya Tanzania.
Msisimko wa mashindano hayo unatazamiwa kuanza kesho kwa pambano kati ya bingwa mtetezi, Yanga itakayovaana na URA.
Prediction Market Apps Lets You Make Money Trading on Outcome of Real World
Events
-
In recent years, a new wave of financial platforms has emerged—prediction
market apps. These platforms allow everyday users to make money trading on
the ou...
2 days ago

No comments:
Post a Comment