Tuesday, December 16, 2008

URA yailiza Mtibwa

Timu ya soka ya URA ya Uganda jana ilianza vyema michuano ya Kombe la Tusker baada ya kuilaza Mtibwa Sugar 1-0 katika mechi ya fungua dimba iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini, Dar es Salaam.

Bao la URA lilizamishwa na Tony Maweje katika dakika ya 50, ambaye alipokea pasi kutoka kwa Eric Obua katika mchezo huo wa kundi A.

Leo mashindano hayo yanatazamiwa kuendelea kwa kuzikutanisha Tusker FC ya Kenya na Prisons ya Tanzania.

Msisimko wa mashindano hayo unatazamiwa kuanza kesho kwa pambano kati ya bingwa mtetezi, Yanga itakayovaana na URA.

No comments:

Post a Comment