Aliyekua nahodha wa timu ya Arsenal William Gallas amenyang'anywa unahodha wa timu ya Arsenal na inasemekana hakusafiri na timu hiyo kwenda Manchester kwa ajili ya pambano lao la leo na Manchester City.
Sababu zilizotolewa za kunyang'anywa unahodha wa Gallas ni maneno aliyosema Gallas alipohojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na mvutano ndani ya Arsenal.
Nafasi hiyo ya unahodha kwenye pambano la leo inaweza kushikiliwa na kipa Manuel Almunia ama mlinzi Gael Glichy.
Katika mahojiano na vyombo vya habari mwanzoni mwa wiki, Gallas alieleza kuwepo kwa kutokuelewana ndani ya timu katika mechi kadhaa ikiwemo ile ya watani wao wa jadi Tottenham waliotoka nao suluhu 4-4 mwezi uliopita.
DSTV Packages Prices In Nigeria (May, 2024)
-
In today’s fast-paced world, where entertainment plays a crucial role in
our lives, having access to a wide array of TV channels is essential. In
Nigeria, ...
1 week ago
No comments:
Post a Comment