Timu ya soka ya URA ya Uganda jana ilianza vyema michuano ya Kombe la Tusker baada ya kuilaza Mtibwa Sugar 1-0 katika mechi ya fungua dimba iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini, Dar es Salaam.
Bao la URA lilizamishwa na Tony Maweje katika dakika ya 50, ambaye alipokea pasi kutoka kwa Eric Obua katika mchezo huo wa kundi A.
Leo mashindano hayo yanatazamiwa kuendelea kwa kuzikutanisha Tusker FC ya Kenya na Prisons ya Tanzania.
Msisimko wa mashindano hayo unatazamiwa kuanza kesho kwa pambano kati ya bingwa mtetezi, Yanga itakayovaana na URA.
Fluent Forms Phone Number Field Not Saving Phone Numbers With Country Code?
Here Is How I Solved It
-
Recently, I ran into a frustrating issue after updating my Fluent Forms
plugin on WordPress. Everything was working perfectly before the update.
But immedi...
1 day ago

No comments:
Post a Comment