Monday, May 25, 2009

Sasa waukataa uharamia Somalia

Kukosekana serikali thabiti nchini Somalia kwasababisha uharamia kustawi

Baada ya kuonekana ni tatizo kubwa Pembe ya Afrika, maharamia wapatao 200 wa Kisomali wametangaza kuacha shughuli hiyo katika mkutano uliofanyika kaskazini mwa nchi hiyo.

Wanachama wa makundi ya maharamia walikutana na viongozi wa mabaraza ya wazeee na wataalam wa Kisomali katika mji wa Eyl, katika jimbo lililojitangazia uhuru la Puntland na wakaahidi kusimamisha mara moja utekaji nyara wa meli.

Mwakilishi wa maharamia hao Abshir Abdullah ameiambia BBC kwamba wataziachilia meli zote wanazoshikilia na watawaachilia huru mabaharia wanaowashikilia .

Maharamia wamekuwa katika chagizo kubwa kutoka kwa wazee wa Kisomali, waliokuwa wakiwashutumu kwa kuiaibisha jamii yao.

Tangu mwaka 1991 Somalia imekuwa haina serikali thabiti hali iliyofanya uharamia ustawi.

Licha ya manowari za kijeshi za kimataifa kupiga doria katika bahari ya Pembe ya Afrika, hali imezidi kuwa mbaya mwaka 2009 ya vitendo vya uharamia wa kuteka meli kushamiri.

Wiki iliyopita serikali ya mpito ya Somalia iliiomba jumuia ya Kimataifa kusaidia kuunda kikosi cha kitaifa cha ulinzi wa bahari katika jitahada za kupambana na uharamia na pia kuwalinda wavuvi kutokana na mashua za uvuvi za kigeni na halikadhalika kuzuia utupwaji wa taka za sumu katika pwani ya Somalia.


Source: BBC

No comments:

Post a Comment