Sunday, February 15, 2009

Mwalimu Asimulia Bakora Alizopata Kutoka Kwa Mkuu Wa Wilaya

Mmoja wa walimu waliocharazwa viboko Jumatano iliyopita asubuhi mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, ni mwalimu Ativus Leonard (33) wa shule ya msingi Katerero.

Akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) juzi, Leonard alisimulia kuwa siku hiyo Mkuu wa Wilaya alifika shuleni kwao na kufanya mkutano na Mkuu wa Shule na walimu wengine.

Katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya aliwaambia kuwa amekuwa akifuatilia walimu wanaochelewa kufika kazini. "Alisoma majina ya walimu waliokuwa wakituhumiwa. Nilikuwa mmoja wao. Nilichelewa mara mbili kufika kazini mwezi uliopita," alikiri Mwalimu Leonard.

Baada ya kusoma majina hayo, kila mmoja aliulizwa atoe sababu za kuchelewa, ndipo yeye alipomwambia kuwa sababu zilitofautiana, yawezekana kuwa za kifamilia au ugonjwa. Ndipo Mkuu wa Wilaya akawambia tabia yao ya kuchelewa ilikuwa inaathiri maendeleo ya shule na kuifanya kushika mkia katika taaluma, jambo ambalo halikubaliki.

"Akasema atatuadhibu sawia. "Kwanza nilidhani anatania. Nikajiambia kuwa hilo halitawezekana...kwa kweli tangu hili litokee nimeshindwa kabisa kufundisha," alisema Mwalimu Leonard. Alisema lakini milango ya chumba cha walimu ilipofungwa na walimu kupangwa tayari kupokea adhabu ya viboko, ndipo mwalimu huyo alipoamini kuwa kumbe linawezekana.

"Walimu wenzetu saba wa kike, walichapwa viganjani, ilipofika zamu yangu, ofisa wa Polisi akaniamuru nilale chini ili nipate adhabu yangu. Nilikataa, lakini alinipiga mtama nikaanguka," alisema Leonard. Alisema wakati akiwa chini, polisi huyo aliendelea kumpiga kwa fimbo kubwa.

"Alinipiga kila mahali; miguuni, kifuani, mikononi. Alipomaliza, nilikwenda hospitalini kwa matibabu. Nilipewa dawa lakini bado nasikia maumivu kifuani," alilalamika. Alisema aliumia miguu pia, lakini kinachomuuma zaidi ni kuwa aliathirika kisaikolojia.

"Hii imenifanya nione aibu kukutana na wanafunzi. Hata kama hawakuniona nachapwa, lakini wanajua nini maana ya kuchapwa," alisema. Alisema ameshindwa kufundisha kwa sababu sasa anajisikia mnyonge mbele ya wanafunzi wake.

"Nimeoa na nina watoto wanne. Mke wangu naye ni mwalimu katika shule tofauti na yangu. Amekasirika kusikia kuwa nimefanyiwa hivi," alisimulia. Alisema mpaka sasa bado ana hasira na ameshikwa na bumbuwazi na haelewi kilichotokea. Pamoja na Mkuu wa Wilaya kuadhibiwa, lakini naye anatafuta jinsi ya kufidiwa na serikali kwa machungu yaliyompata.

Naye Phinias Bashaya, anaripoti kutoka Bukoba, kwamba siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kumvua madaraka Mnali, Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Kagera, kimekiri kuwa baadhi ya walimu walisingizia kucharazwa viboko na mkuu huyo, ili kuwaunga mkono walimu wenzao.

Kauli hiyo imekuja baada ya viongozi wa chama hicho kuombwa kuthibitisha idadi halisi ya walimu waliocharazwa viboko baada ya vyombo vya habari kuripoti idadi tofauti ya walimu waliodaiwa kukumbwa na tukio hilo.

Wakizungumza katika ofisi zao mjini hapa jana, Katibu wa Mkoa, Aaron Masalu, alisema waliupokea kwa furaha uamuzi wa Rais na kuupongeza na kukiri kuwa walitembelea shule zilizohusika na tukio hilo na kuambiwa na walimu kuwa hata ambao hawakucharazwa nao waliingia katika mkumbo.

Alisema baada ya kugundua hali hiyo ya kutofahamu idadi halisi ya walimu waliocharazwa huku walimu wote wakidai kuchapwa, ilibidi viongozi hao na walimu wakubaliane waandaliwe walimu wenye uwezo wa kujieleza na kufafanua mazingira ya tukio lenyewe hata kama hawakuhusika na adhabu hiyo.

Akitetea hali hiyo, Mwenyekiti wa CWT, Dauda Bilikesi, alitolea mfano wa mtoto anayeweza kukunja ngumi kumtishia mzazi wake, hali ambayo alisema lazima itafsiriwe kuwa mtoto huyo alimpiga mzazi wake hata kama hakumgusa.

Naye Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Bukoba Vijijini, Gosbert Mashasi, mbali na kuungana na viongozi wenzake, pia alikiri upungufu miongoni mwa walimu na kusema wanaipongeza hatua iliyochukuliwa na Rais dhidi ya Mkuu wa Wilaya. Wakitoa maoni yao kuhusu hatua ya kuvuliwa madaraka kwa Mkuu wa Wilaya baadhi ya wakazi wa Kagera wakiwamo viongozi, walikuwa na maoni tofauti.

Florian Kaiza (34) mfanyabiashara wa mjini hapa aliupongeza uamuzi wa Rais akisema unafaa kwani kilichofanyika ni udhalilishaji mkubwa dhidi ya walimu. Aliongeza kuwa walimu walishapata jibu walilolihitaji na kuwaasa kuwa hakuna haja ya kuandamana badala yake watulie na wafanye kazi bila kuvunjika moyo, akiungwa mkono na Diwani wa Kasharunga, Muleba, Ponsian Rweyemamu (43), aliyeongeza kuwa yapo masuala mengi nchini yanayohitaji uamuzi wa haraka kama alivyofanya Rais.

Akizungumza kwa simu, Mwalimu Leonard ambaye pia ni Katibu wa Chama cha walimu kwenye shule hiyo, alisema alifarijika na uamuzi dhidi ya Mkuu wa Wilaya na kusema sasa walimu watulie na kufanya kazi. Tofauti na wengine kijana aliyejitambulisha kwa jina la Kraish Ally (32) wa mjini hapa, alisema Mkuu wa Wilaya ameonewa, akidai kuwa walimu wamewachosha wazazi kwa utoro na kutofundisha.

Alisema walimu wamekuwa wa kwanza kuvunja haki za watoto ambao wanastahili kufundishwa na badala yake kutanguliza miradi yao aliyosema inaendeshwa hata shuleni wakati wa masomo. Juzi Rais Kikwete alichukua hatua ya kumvua madaraka Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuvunja Kanuni ya Sheria za Utumishi wa Umma na kuidhalilisha Ofisi na Mamlaka ya Ukuu wa Wilaya.



Zimbabwe bado yazongwa na mizengwe

Bw Bennet ni mwanasiasa aliyewahi kuwa mkulima

Polisi nchini Zimbabwe wamemfungulia mashtaka ya uhaini mwanachama mwandamizi wa chama cha MDC kinachoongozwa na waziri mkuu Morgan Tsvangirai, chama hicho kimeeleza.

Roy Bennett, mteuliwa wa kiti cha naibu waziri wa kilimo, alifunguliwa mashtaka saa chache baada ya kuapishwa kwa baraza jipya la mawaziri kwa mujibu wa mkataba wa kugawana madaraka, chama cha MDC kimeeleza.

Taarifa ya chama hicho imeelezea mashtaka hayo kuwa ni kashfa na yenye mwelekeo wa kuchochewa kisiasa.

Awali, sherehe ya kuapishwa kwa baraza hilo ilikumbwa na utata kuhusu mgawanyo wa viti vya mawaziri.

Kwa mujibu wa mkataba wa ugawanaji madaraka ulioafikiwa baada ya miezi mingi ya majadiliano tangu uchaguzi uliozua mzozo, chama cha Zanu-PF kinachoongozwa na rais Robert Mugabe kitapata viti 15 na makundi mawili ya MDC yanayopingana yatagawana viti 16 serikalini.

Lakini wanachama saba zaidi wa Zanu-PF walijitokeza ikulu mjini Harare kuapishwa.Swala hilo lilipatiwa ufumbuzi baada ya majadiliano makali yaliyofanyika kwa faragha.


Source: BBC

If the shoe fits: World's shortest man meets world's biggest shoe

The world's shortest man He Ping Ping took Tokyo by storm while visiting the city on Friday to launch the 2009 edition of the Guinness Book of World Records.

Mr Ping Ping, who was born with a form of dwarfism and is 74.1 cm tall and 7kg in weight, easily slipped into the shoe of the world's tallest man. He has been officially named by the book as the world's shortest man.

He lives in Inner Mongolia, China, and Tokyo is just one of many places around the world he has visited, including London and New York.

He Ping Ping


He Ping Ping holds a shoe of the world's tallest person at The Guinness World Records Museum in Tokyo on Friday


Mr Ping Ping said: 'I'm not particularly envious of someone who is tall. If you're tall it is hard to move and it's very inconvenient,' according to reports.

'I can weave my way through tight spots if I'm short. It's much better to be short,' he added.

Mr Ping Ping


Mr Ping Ping stands in front of a statue of the world's tallest person at the exhibition

Mr Ping Ping

Surrounded by photographers at a press conference in Tokyo


He is friends with another title holder, Bao Xishun, who was once the world's tallest man at 2.36m. Mr Xishun also lives in China's Inner Mongolia.

The current title holder for world's tallest man is Leonid Stadnyk, a 37-year-old former veterinarian from the Ukraine. At 2.57m, he is taller than Mr Xishun by 0.22cm.

Friends: Mr Ping Ping meeting with Bao Xishun in 2007. Mr Xishun was once the world's tallest man


Source: Daily Mail Uk

If the shoe fits: World's shortest man meets world's biggest shoe

The world's shortest man He Ping Ping took Tokyo by storm while visiting the city on Friday to launch the 2009 edition of the Guinness Book of World Records.

Mr Ping Ping, who was born with a form of dwarfism and is 74.1 cm tall and 7kg in weight, easily slipped into the shoe of the world's tallest man. He has been officially named by the book as the world's shortest man.

He lives in Inner Mongolia, China, and Tokyo is just one of many places around the world he has visited, including London and New York.

He Ping Ping

He Ping Ping holds a shoe of the world's tallest person at The Guinness World Records Museum in Tokyo on Friday

Mr Ping Ping said: 'I'm not particularly envious of someone who is tall. If you're tall it is hard to move and it's very inconvenient,' according to reports.

'I can weave my way through tight spots if I'm short. It's much better to be short,' he added.

Mr Ping Ping

Mr Ping Ping stands in front of a statue of the world's tallest person at the exhibition

Mr Ping Ping

Surrounded by photographers at a press conference in Tokyo

He is friends with another title holder, Bao Xishun, who was once the world's tallest man at 2.36m. Mr Xishun also lives in China's Inner Mongolia.

The current title holder for world's tallest man is Leonid Stadnyk, a 37-year-old former veterinarian from the Ukraine. At 2.57m, he is taller than Mr Xishun by 0.22cm.

Friends: Mr Ping Ping meeting with Bao Xishun in 2007. Mr Xishun was once the world's tallest man


Source: Daily Mail Uk

Wednesday, February 11, 2009

Taifa Stars, Zimbabwe Nguvu Sawa

HUKU zikijiandaa kwa fainali za Afrika za wachezaji wa ligi za ndani, CHAN, timu ya Taifa Stars na wageni wao, Zimbabwe zimeshindwa kukonga nyoyo za mashabiki wengi waliofurika Uwanja wa zamani wa Taifa, Dar es Salaam na kutoka suluhu.

Katika mchezo huo ambao ulishuhudiwa na maelfu ya mashabiki wengi wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete aliyeingia uwanjani hapo kushuhudia , yeye ndiye aliyeshangiliwa zaidi.

Hata hivyo, kwa kiasi kikubwa cha kipindi cha kwanza, pia kile cha pili, mchezo huo ulionyesha kupooza kwa kukosa kasi ya kuridhisha.

Stars, kwa upande wao ndio walioanza kulikaribia lango la Wazimbabwe, wakianza kutia matumaini kwa mashabiki wao tangu dakika ya tatu ya mchezo, kisha tena dakika ya tano na saba kuwa wangeibuka na ushindi, lakini walijikuta wakikosa mbinu za kuweza kukwamisha mipira wavuni.

Baadhi ya mipira ya kona katika muda huo, ama ilikosa waunganishaji au mingine ikiokolewa na kipa wa Zimbabwe, Willard Nyamatera aliyepangua shuti kali la dakika ya 12, la beki Shadrack Nsajigwa.

Phillip Marufu wa Zimbabwe, alimjaribu kipa Shaaban Dihile kwa shuti, dakika ya 13, lakini kipa huyo alikaa chonjo na kulidaka.

Stars ilipata pigo dakika ya 22 baada ya kiungo wake, Nizar Khalfan kuumia na kutoka nje na nafasi yake kuchukuliwa na Mwinyi Kazimoto.

Katika mchezo huo, mabeki wa Zimbabwe walimkamia na kumchezea rafu, kumkwatua mshambuliaji Mrisho Ngassa. Jaribio la dakika ya 25 la Haruna Moshi ambaye aliachia mkwaju mkali, lilizimwa tena na kipa wa Zimbabwe.

Ukosefu huo wa umakini uliendelea kuwasumbua wachezaji wa Stars huku kiungo mgeni, Kazimoto akiungana na Jerry Tegete katika kukosa nafasi nzuri ya kufunga bao, dakika ya 40.

Kwa upande wao, mashabiki nao walisikika wakipiga kelele za kumtaka kocha, Marcio Maximo ampumzishe Tegete kutokana na kupooza kwa kiasi kikubwa katika mchezo huo.

Kipindi cha pili, Maximo aliwapumzisha Tegete, Kazimoto na kuwaingiza Mussa Hassan Mgosi na Kigi Makassi huku Zimbabwe pia ikifanya mabadiliko kadhaa katika kikosi chake, ambayo hata hivyo hayakusaidia kubadili mchezo huo ambao uliendelea kupooza.

Mashambulizi mengi ya Stars langoni mwa Zimbabwe ambayo hayakuwa na malengo yalizimwa na mabeki wa Zimbabwe na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa suluhu 0-0.

Kocha wa Zimbabwe, Sunday Marimo alieleza baada ya mchezo huo kuwa vijana wake walijitahidi kucheza vizuri na kueleza kuwa Stars wameonyesha kiwango cha kuridhisha, lakini mchezo ulikuwa mgumu. Marimo alieleza kutiwa moyo na timu zote mbili kuwa zitakwenda Ivory Coast zikiwa zimekamilika.

Kocha huyo alikuwa kivutio baada ya filimbi ya mwisho alipowaita wachezaji wa pande zote mbili na kuwapa mazoezi ya viungo.

Maximo aliwasifu wachezaji wake kwa kucheza vizuri katika mchezo huo uliokuwa mgumu kutokana na aina ya uchezaji wa wapinzani wao walioweka viungo wengi zaidi na kuwanyima nafasi ya kupenya na kucheza mchezo wao wa kawaida.


Monday, February 9, 2009

Svelte Katy Perry and voluptuous Leona Lewis lead the glamour stakes at the Grammys

Singers Leona Lewis and Katy Perry may be like chalk and cheese, but they were both clear winners in the style stakes at last night's Grammy Awards.

Golden-haired singer Leona, 23, wore a floor length gown which matched her honey skin tone by designer Randi Rahm.

Studded with golden crystals, the halter necked gown clung to her womanly curves as she oozed glamour on the Grammys red carpet.

While Katy, 24, who recently split from Gym Class Heroes boyfriend Travis McCoy showed off a very slim silhouette in a sugar pink strapless pleated gown.

Golden girls: Leona Lewis emerged as a clear winner in the style stakes along with Katy Perry at the 51st Grammy Awards in Los Angeles last night

Playing it safe: Brit singers Duffy and Adele opted for unadventurous black cocktail dresses - Duffy's vintage-looking number is by celebrity favourite Alberta Ferretti

However, despite her winning look, Leona was the biggest British loser of the night, walking away empty handed from her three nominations.

While winners Adele and Duffy played it safe in classic black cocktail dresses, the X Factor winner and the I Kissed A Girl singer opted for full on glamour for the prestigious event.

Katy said: 'So I did have a previous dress ready to go tonight that might have ended up `worst dressed.' But it came in the mail, because I had it custom-made of course — because I didn't want anyone wearing that dress, ever — and it wasn't right. And it was the day before the Grammys.'

Full length and fabulous: Country music stars Sheryl Cole, Carrie Underwood and Taylor Swift all opted for stunning floor length gowns

Her stylist found the pink frock by Lebanese designer Basil Soda.

She said: 'I gotta ship the dress back to Lebanon tomorrow. But I feel great. I'm so glad there's always a Plan B.'

Many stars were picture-perfect at the event held last night at the Staples Centre in Los Angeles.

Both Gwyneth Paltrow and Paris Hilton opted for minidresses but Gwyneth decided to keep her well-honed limbs under wraps in a pair of frumpy grey tights on this occasion

Welsh singing sensation Duffy, who took home the award for Pop Vocal Album for her best-selling disc Rockferry, also went with a last-minute choice - an Alberta Ferretti black cocktail dress with a jewelled neckline and a sheer asymmetrical pattern at the bust.

A safe choice for the retro-influenced singer, who prefers a vintage-inspired look.

While singer Sheryl Crow looked uber-glamorous in a slinky one-shoulder electric blue gown by Toni Maticevsk, as did country singer Carrie Underwood in a gold beaded tulle slip gown from Zuhair Murad.

Young singer Taylor Swift embraced her sexier side in a plunging strappy black number by Kaufman Franco.

Made it back: Jennifer Hudson chose a white, silver and black statement dress by designer Roland Mouret for her return to the spotlight in front of the star-studded industry audience

Singer Jennifer Hudson - another winner on the night - wore a white, silver and navy colour-blocked cocktail dress by Roland Mouret for her emotional comeback in front of the star-studded industry audience.

It was an unusual choice for the singer, but showing off a slimmer silhouette, she more than
did the statement dress - with its white high neck bodice, pleated peplum around the waist, and dark navy pencil skirt - justice.

Keeping her hair simple with a side-swept ponytail, a pop of colour came from her teal blue Christian Louboutins.

Out of this world: Winner Estelle and nominee M.I.A opted for outlandish mini dresses

British singer Estelle, who took home a Grammy for her duet with Kanye West, wore one of the night's more outlandish outfits along with fellow nominee M.I.A.

But she won no points for her space-age silver get-up - complete with peep-toe boots.

While heavily pregnant M.I.A. performed her hit “Paper Planes” prancing around in a Henry Holland polka-dot mini with a sheer midriff, and looked very comfortable doing so.

In general, most performers played it safe with some observers commenting that the show lacked the free spirit that typically sets the Grammys apart from other shows during the crammed awards season.

Mini adventures: Singers Robyn, left, Solange Knowles and former Destiny's Child singer Letoya Luckett opted for shorter lengths

'It seems a lot more tame, tamer than usual,' said Kamarake. The rappers in particular toned down the flash



"They could have risked being too ostentatious in this time, rubbing it in people's faces when people are sitting around the table figuring how they're going to put dinner on the table, said Memsor Kamarake, fashion editor at US style and music magazine Vibe.

Singers Robyn, Solange Knowles and Letoya Luckett formerly of Destiny's Child opted for fashionable mini dresses to show off their legs.

Robyn also held a cute custom-made jewelled handbag in the shape of robin bird.

Miley Cyrus shrugged off the row surrounding her recent questionable 'slanty-eyed' pictures to appear at the show.

She added some youth to her mature Max Azria gown with stacked diamond bracelets by Mimi So in a mature look for the teen sensation.

Socialite and reality television star Kim Kardashian was a surprise hit on the red carpet in a sculptural mini dress which covered her most well-known asset - her bottom.

Sculpted: Kim Kardashian opted for a bottom-concealing sculptural mini-dress in dove grey by Toni Maticevski

Teen sensation Miley Cyrus opted for grown up glamour in a full length Herve Leger by Max Azria gown



Source: Daily Mail Uk.

Saturday, February 7, 2009

Polisi yaua watano Madagascar

Watu waendelea kupoteza maisha Madagascar

Taarifa kutoka Madagascar, zinasema takriban watu watano wameuawa baada ya askari polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji wa upinzani katika mji mkuu Antananarivo.

Hata hivyo taarifa nyingine zinasema watu waliouawa wanafikia ishirini na watano.

Kumekuwa na upinzani mkali nchini humo dhidi ya hatua ya kufukuzwa Meya wa mji wa Antananarivo Andry Rajoelina, ambaye amekuwa katika harakati za kuwania madaraka na rais wa nchi hiyo.

Meya aliyetimuliwa amekuwa akimtuhumu rais Marc Ravalomanana kwa kufuja fedha za umma na kuendeleza udikteta.

Kwa mujibu wa afisa mmoja mwandamizi wa jeshi la polisi aliyenukuliwa na shirika la habari la Reuters, inawezekana watu 25 wameuawa.

Waandamanaji walikuwa wanaelekea katika makazi ya Rais Ravalomanana ndipo polisi wa kuzuia ghasia walipofyatua risasi.

Mapema wakati wa maandamano hayo yaliyohudhuriwa na watu 20,000, wafuasi wa Meya wa zamani walimtangaza kuwa ni kiongozi wa serikali ya mpito ya nchi hiyo.

Bwana Rajoelina alifutwa kazi na serikali siku ya Jumanne na nafasi yake imechukuliwa na Guy Randrianarisoa.

Bwana Rajoelina, ambaye amefanikiwa kuisumbua serikali kutokana na utendaji mbovu, amesema ataunda serikali ya mpito kama rais President Marc Ravalomanana hatojiuzulu.

Madagascar, ambacho ni kisiwa kikubwa cha nne duniani, kwa muda mrefu kimekuwa kikitembelewa na watalii na kituo cha makampuni mengi ya kigeni, hivi sasa kimo katika harakati za kutafuta mafuta, madini ya shaba na uranium.


Source: BBC

Friday, February 6, 2009

Yanga yanusa ubingwa ligi kuu Tanzania Bara

Bao la Jerry Tegete, dakika ya 57 limetosha kuiwezesha Yanga kuvunja ukuta mgumu wa Moro United na kuiacha timu hiyo ikihitaji mechi mbili za dakika 180 ili kujitangazia ubingwa.

Mpira wa Mrisho Ngassa kuelekea lango la wapinzani wao ulisababisha piga nikupige langoni mwa Moro United na kumpa nafasi Tegete kuandika bao pekee na muhimu,huku akimwacha kipa Haji Macharazi akichupa bila mafanikio.

Awali, United ilipania vilivyo kuchelewesha azma ya Yanga kujitangaza bingwa mapema baada ya kuigomea kwa dakika 45 za mchezo huo mkali uliofanyika jana katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ikicheza chini ya ukocha wa mchezaji na beki wa zamani wa Yanga, Fred Felix Minziro, Moro United ambayo ipo katika hatari ya kushuka daraja ilimudu kwa muda huo kuyazuia mashambulizi ya wachezaji wa Yanga na hivyo kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Mchezo huo mkali ulishuhudia timu hizo zikishambuliana na kusaka mabao na pointi, lakini safu za ulinzi za timu hizo zilikaa imara na kujaribu kuondosha hatari zote. Ukuta wa Moro United uliokuwa chini ya beki wa zamani wa Simba, Said Kokoo ulisimama imara na kuwazuia kwa muda washambuliaji wa Yanga.

Katika kipindi hicho, kila timu ilijitahidi kusaka bao, lakini bila mafanikio, ingawa kwa kiasi kikubwa Yanga ilionyesha zaidi dhamira ya kupata ushindi na kuhitaji ushindi katika mechi mbili ili kujitangaza bingwa.

Kwa upande wao, vijana wa Moro United walioko nafasi ya tisa ya msimamo wa ligi hiyo yenye timu 12 walikuwa imara na kuzima kiu ya washambuliaji wa Yanga.

Mchezaji wa zamani wa Yanga, Kudra Omari alikaribia kuipa bao timu yake dakika ya tatu ya mchezo huo kwa shuti kali ambalo hata hivyo lilipaa na kutoka nje.

Naye Tegete wa Yanga, dakika ya 11 alizubaa na kushindwa kupachika wavuni mpira baada ya pasi maridhawa ya Mrisho Ngassa huku Boniface Ambani akichezea nafasi, dakika 25 na 30 kwa mashuti ambayo yalitoka nje.

Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Nizar Khalfan aliikosesha bao timu yake, dakika ya 43 kwa shuti kali ambalo lilipanguliwa na kipa Mzungu Obren Curkovic.

Kipindi cha pili, kocha Dusan Kondic aliwapumzisha Vincent Barnabas na Tegete na kuwaingiza Mike Baraza na Shamte Ally na Moro United ikimpumzisha Thomas Maurice na kuingia Samwel Ngassa, mabadiliko ambayo hayakubadili sura ya mchezo.

Baraza aliingia katika orodha ya waliokosa mabao baada ya dakika 76 za mchezo huo baada ya kubakia na kipa Macharazi na kukosa mbinu za kufunga bao kutokana na krosi ya Ngassa, lakini mpira huo ukampita.

Kosa kosa ziliendelea kwa pande zote mbili, huku Kudra akitikisa nyavu dakika ya 80, lakini mwamuzi Owden Mmbaga alilikataa bao hilo kwa madai ya kuotea.

Minziro alieleza baada ya mchezo kuwa timu yake ilistahili sare ya bao 1-1, lakini uamuzi mbovu umeiathiri. Kocha huyo alionyesha hasira na kukaribia kumwaga chozi baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo huo.

"Bao la Kudra lilikuwa safi, inashangaza kuona mwamuzi amelikataa. Waamuzi wapunguze ushabiki wao, vinginevyo wanaimaliza soka ya Tanzania," alidai.

Dusan Kondic wa Yanga alieleza kuwa hawezi kuuzungumzia mchezo wowote hadi abakiwe na mchezo mmoja kabla ya kutangaza ubingwa.

Ligi hiyo imeahirishwa kwa muda hadi Machi ili kuipa nafasi timu ya taifa, Stars kujiandaa na michuano ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika nchini Ivory Coast baadaye mwezi huu.

Thursday, February 5, 2009

Arshavin's Secret Women's Clothing





















It seems the new Arsenal #23 has a little secret that he doesn't want his new teammates in London to discover. Although Andrei Arshavin began studying chemical technology at the University of Technology and Design in St Petersburg, he later switched to the clothes designing department because there was a higher ratio or girls enrolled in their classes. But it seems that the young Russian excelled at designing clothes, and now he has his very own line... of women's clothing. His range is quite popular with Russian women and includes everything from dresses to active wear.



















Perhaps his teammates could get their WAGs to start buying his stuff and by next season he'll be all other London Fashion Week. Or they could bust on him incessantly. Probably the latter.



pictures via dailymail

Wednesday, February 4, 2009

New brunette Scarlett Johansson outshines drab blonde Jennifer Aniston on the red carpet

A newly-brunette Scarlett Johansson won the battle of the red carpet last night as she joined her A-list co-stars at the world premiere of their new movie He's Just Not That Into You.

Teaming her new dark locks with a figure-hugging floral Oscar de la Renta strapless dress, Scarlett outshone Jennifer Aniston, who went for an uninspired Burberry trouser suit in her signature colour black.

Explaining her recent change from her usual blonde shade, the 24-year-old said: 'It's part of being a girl. We get to change up our thing and confuse everybody.'

Scarlett Johansson

Because I'm worth it: Scarlett Johansson flicks her new long brunette hairstyle for the cameras at her latest film premiere last night


New look: Scarlett went for full glamour in a floor-length floral gown by Oscar de la Renta and poker-straight hair
Scarlett Johansson


Bombshell: Johansson's usual blonde hairstyle

The two women joined their co-stars Drew Barrymore, Ginnifer Goodwin and Jennifer Connelly at the star-studded screening of the romantic comedy at the Grauman's Chinese Theater in Hollywood.

Clearly wanting to stand out from each other, all five women went for dramatically different fashion styles.

In the sexiest outfit of the night, Oscar winner Connelly, 38, showed off her long legs in a green Balmain mini-dress.

Giving a nod to the trend for bondage-style shoes, Connelly wore a £1,335 pair of Balmain studded crystal high-heels sandals - the same worn by Bond girl Gemma Arterton at the London premiere of Quantum Of Solace last year.

Drew, 33, also went for high-fashion with a strapless black mini-dress with oversized bow.

Walk The Line star Ginnifer, 30, looked short and sweet in a burnt orange mini-dress and matching strappy sandals.

The premiere marked one of Ginnifer's first public appearances since she split from American Pie actor Chris Klein - ex-fiance of Katie Holmes - in December.

Joining Ginnifer as the only two single stars was Drew, who is revelling in her single status after years of monogamy.

Despite splitting from her He's Just Not That Into You co-star Justin Long (who also attended last night) in July, the couple remain on good terms and have been spotted chatting to each other on the publicity round for the movie.


Lady in black: Jennifer Aniston dressed in an uninspiring Burberry trouser suit
Jennifer Aniston and Scarlett Johansson


A somberly dressed Jennifer Aniston greets co-star Scarlett Johansson


Statement style: Drew Barrymore opted for this season's must-have, an oversized bow, while Jennifer Connelly showed off her pins in a green Balmain mini-dress

Also at the screening were the male stars Ben Affleck, Kevin Connolly and Bradley Cooper.

With so many stars of the ensemble piece at the premiere, Connelly, Aniston and Scarlett's partners chose to stay away.

Connelly has been married to English actor Paul Bettany for five years, while Scarlett wed in September.

Silencing recent reports Aniston, 39, has split from John Mayer, the musician has been taking to his Twitter online messaging service to joke about their relationship.

Scarlett Johansson

Here come the girls: Drew, Connelly, Aniston, Ginnifer and Scarlett buddy up for the cameras


Ginnifer Goodwin looked fiery in burnt orange, while Ben Affleck was dapper in a black suit and tie

Writing two days ago, he said: 'Welding an engagement ring for my girlfriend.'

On Sunday, the couple spent the day together watching the American Football final at a friend's Super Bowl party in Los Angeles.

As well as a new film coming out this week, Aniston is gearing up to mark her 40th birthday next Wednesday.

He's Just Not That Into You is based on the self-help guide by Greg Behrendt and Liz Tuccillo, which inspired an episode of Sex And The City.

The film tells the story of a group of twenty and thirtysomethings living in Baltimore, whose complicated love lives interlink and the female characters spend their time trying to interpret what their men are thinking.

The film is set for release in the UK this weekend.

Brunette V Blonde: Other stars who have tried both looks


Lily Allen last month as a brunette and, R, last May with blonde locks

Cameron Diaz has also experiment with darker and lighter shades

Gwyneth Paltrow has dabbled with brunette and blonde hair styles


Source: Daily Mail Uk.

Tuesday, February 3, 2009

Maximo atangaza kikosi cha Stars chenye wachezaji 27

Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ‘Taifa Stars’ Marcio Maximo amewaita wachezaji Mwinyi Kazimoto na Zahoro Pazi kwenye kikosi chake kwa ajili ya kujiandaa na fainali za michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika Ivory Coast kuanzia Februari 22 mwaka huu.

Kocha Maximo alitangaza kikosi chake Dar es Salaam jana, kikiwa na wachezaji 27 na kinatarajiwa kuingia kambini jijini hapa kesho kuanza maandalizi ya fainali hizo.

Zahoro Pazi anayechezea Mtibwa Sugar ambaye ni mtoto wa kipa wa zamani wa Simba ya Dar es Salaam, Idd Pazi ‘Father’, ndiye aliifunga Yanga bao pekee lililopatikana katika mchezo wa Kombe la Tusker hatua ya makundi Desemba mwaka jana, ambalo lilifanya matokeo ya kundi hilo la Yanga lililokuwa pia na timu ya URA ya Uganda yapatikane kwa njia ya kura, baada ya timu zote kuwa na pointi sawa.

Yanga ilitolewa katika utaratibu huo, hivyo Mtibwa na URA kutinga nusu fainali. Kazimoto ni kiungo mahiri wa JKT Ruvu, ambaye alijizolea sifa katika michuano ya Kombe la Taifa Mei mwaka jana iliyofanyika Dar es Salaam, akichezea timu ya Mkoa wa Pwani.

Hivi sasa Kazimoto anachezea JKT Ruvu na ni miongoni mwa wachezaji wanaong’ara katika Ligi Kuu Tanzania Bara. Maximo alisema katika kikosi hicho cha wachezaji 27, amewarudisha baadhi ya wachezaji waliokuwa kwenye kikosi hicho na kuchezea michuano mbalimbali, lakini hawakuwemo katika timu iliyokuwa ikiwania kufuzu fainali za CHAN.

Aliwataja wachezaji hao kuwa ni Erasto Nyoni na Salvatory Ntebe ambao sasa wanachezea Azam ya Dar es Salaam, wakiwa wameongezwa katika usajili wa dirisha dogo, ambapo wakati wa michuano ya CHAN mwaka jana walikuwa wakichezea Vital’O ya Burundi.

Wachezaji wengine ambao hawakuwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ kilichoshiriki michuano ya Chalenji, lakini wapo katika kikosi cha Taifa Stars ni beki Amir Maftah (Yanga), kiungo Jabir Aziz (Simba) na Uhuru Selemani (Mtibwa Sugar).
Pia katika kikosi chake, Maximo amemtema beki Meshack Abel wa Simba, ambaye alishiriki katika kuiwezesha Stars kufuzu fainali hizo. Wachezaji walioitwa tena katika kikosi hicho ni makipa Deogratius Boniventure ‘Dida’ kutoka Simba, Shaban Dihile (JKT Ruvu) na Farouk Ramadhan (Miembeni).

Walinzi ni Shadrack Nsajigwa, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga), Salum Sued (Mtibwa), Kelvin Yondani na Juma Jabu (Simba) Viungo ni Nurdin Bakari, Geofrey Bonny, Athumani Iddi, Abdi Kassim ‘Babi' (Yanga), Henry Joseph, Haruna Moshi (Simba) na Shaban Nditi wa Mtibwa.
Wakati washambuliaji ni Mussa Hassan ‘Mgosi’ (Simba), Jerry Tegete, Mrisho Ngassa, na Kigi Makasi kutoka Yanga, ambapo alisema atateua wachezaji 23 wa kwenda nao Ivory Coast.

Akizungumzia suala la kuitwa nahodha wa kikosi hicho, Henry Joseph ambaye yuko nchini Norway akifanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa, Maximo alisema mchezaji huyo akifuzu ataondolewa kikosini, lakini akikwama atakuwemo.

“Ukifanya uteuzi wa wachezaji chipukizi inakulazimu uwe na umakini wa hali ya juu, kwani chipukizi hao huwa na vipaji bila uzoefu, hivyo itawachukua muda kupata uzoefu kama wenzao,” alisema Maximo.

Pia alizungumzia suala la utaratibu wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuwapima wachezaji kubaini endapo wanatumia dawa za kuongeza nguvu, ikiwemo bangi na kusema kuwa suala hilo ni utaratibu wa kawaida na anaufurahia, kwani unafanya wachezaji wawe kama wa kulipwa na kuishi maisha ya kimichezo.

Pia kocha huyo alisema michuano hiyo ya CHAN itakuwa migumu kwa Stars, ambayo haipewi nafasi kubwa ya kufanya vyema, lakini aliwataka wadau wa soka kutambua kuwa kutopewa nafasi huko sio sababu ya kutofanya vizuri.

“Ni kweli hatupewi nafasi ya kufanya vyema kwenye CHAN ukilinganisha na timu kama Ghana na Senegal ambazo zina wachezaji wazoefu wa ndani ambao baadhi yao hata wamecheza kombe la dunia, lakini pamoja na hayo sisi sio vibonde,” alisema kwa msisitizo Maximo.

Stars itacheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Zimbabwe Februari 11, Dar es Salaam, ikiwa ni maandalizi ya fainali hizo. Katika kikosi cha jana, Maximo ameendelea kumuweka kando kipa mahiri nchini Juma Kaseja, ambaye wadau wengi wa soka wamekuwa wakipiga kelele awepo katika kikosi hicho.

“Sina tatizo na timu, naamini ipo siku nitacheza, bado umri wangu unaruhusu, najiamini nina uwezo wa kucheza, ipo siku nitawatumikia Watanzania,” alisema Kaseja jana kwa njia ya simu alipozungumza na HabariLeo. Kauli hiyo pia iliungwa mkono na Kocha Mkuu wa Villa Squad, Kenny Mwaisabula, aliyesema hajui kosa ambalo kipa huyo amelifanya kiasi cha kutoitwa katika kikosi hicho.

“Huyu bwana mdogo hakuua, sasa kosa gani ambalo halistahili kusamehewa? “Nadhani kulikuwa na haja ya kumsaidia mwalimu maana ni kwa manufaa ya Watanzania wote,“ alisema Mwaisabula.


Djibril Cisse Looks Ridiculous… Per Usual


While attending the Pussycat Dolls concert in Manchester, Cisse actually left his home wearing this. Does he have no friends? Where was Jude? Ugh.

It’s been reported that Manchester City stars, Shaun Wright-Phillips and Robinho were also at the concert.


picture via The Sun

JKT Ruvu yaishika koo Simba, yaambulia sare

PAMOJA na kuendeleza imani za ushirikina na kuzuia magari ya mashabiki yasiingie uwanjani kabla ya basi la wachezaji wao, haikutosha kuifanya Simba kupata pointi zote tatu baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 na JKT Ruvu katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana.

Vituko vilitawala kwenye lango kuu huku viongozi wa Simba wakizuia magari yote kuingia kwenye geti hilo kwa madai kuwa walikuwa wanafanya mambo yao na kusababisha usumbufu kwa mashabiki waliofika uwanjani hapo na magari.

Baada ya tukio hilo timu ya JKT Ruvu walitumia geti dogo kuingia uwanjani wakitokea eneo la jukwaa lenye rangi nyekundu na baadaye wakiingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

Simba iliyoanza kipindi cha kwanza kwa kasi na kufanya mashambulizi mengi golini kwa JKT, lakini washambuliaji wake Ulimboka Mwakingwe, Haruna Moshi pamoja na Musa Hassan Mgosi walipoteza nafasi katika dakika ya 34, 38 na 40.

Maafande wa JKT Ruvu walijibu mapigo katika dakika ya 41 na kupata bao la kuongoza kupitia Haruna Adolf aliyetumia vizuri uzembe wa mabeki wa Simba na kupiga shuti lililomshinda kipa Amani Simba na kufanya matokeo kuwa 1-0 hadi mapumziko.

Kipindi cha pili Simba walionekana kuwa makini zaidi na kufanya mashambulizi mengi zaidi golini kwa JKT katika dakika ya 47, Ulimboka Mwakingwe alishindwa kumalizia pasi nzuri aliyotegenezewa na Haruna Moshi 'Boban'.

Vijana hao wa Mtaa wa Msimbazi waliendeza kasi hiyo na kufanikiwa kupata penalti baada ya beki Buji Seleman kunawa mpira kwenye eneo la hatari.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Musa Hassani Mgosi alitumia vyema nafasi hiyo kwa kufunga bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 65 ya mchezo.

Mwisho wa mchezo huo kocha Partick Phiri aliwalaumu washambuliaji wake kwa kusoka umakini kwenye umaliziaji na kuahidi kulifanyia kazi tatizo hilo.

Naye kocha Charles Kilinda wa JKT Ruvu amemlalamikia mwamuzi wa mchezo huo Othman Kazi kwa kutokuwa makini na kuonyesha upendeleo zaidi kwa Simba.

Kwa matokeo hayo Simba imebaki kwenye nafasi ya pili na pointi zake 24 huku Yanga akiwa kileleni na pointi zake 39 wakati ligi inapoingia kwenye mapumziko leo hadi Marchi 14 kupisha maandalizi ya Taifa Stars kwa ajili ya fainali za mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) yatakayoanza kutimua vumbi baadaye mwezi huu.


Monday, February 2, 2009

Theluji nzito yavuruga usafiri London

Usafiri wakwama London kutokana na theluji nzito

Maelfu ya wakaazi wa London wameshindwa kwenda kazini leo kutokana na theluji nzito iliyoanguka usiku kucha na usafiri wa mabasi na treni kutatizika na theluji inaendelea kuanguka.

Usafiri wote wa mabasi na treni ziendazo chini ya ardhi hasa Circle, Hammersmith & City na Waterloo & City zimesimamishwa.

Njia zote za kurukia ndege isipokuwa moja tu katika uwanja wa ndege wa Heathrow zimefungwa. Uwanja wa ndege wa London bado umeendelea kufungwa.

Theluji hiyo nzito imesababisha ndege ya shirika la ndege la Cyprus kuteleza na kutoka katika njia wakati ikielekea kuegesha katika uwanja wa Heathrow na ikajikita katika eneo la nyasi.

Kwa mujibu wa Mamlaka inayosimamia uwanja wa ndege wa Heathrow abiria wote walikuwa salama katika tukio hilo lililotokea mapema saa mbili na dakika ishirini asubuhi.

Mamlaka hiyo imearifu ndege hiyo ilikuwa ni ya mwisho kuwasili kabla sehemu za kurukia na kutua ndege hazijalazimika kufungwa.

Shirika la ndege la Uingereza-British Airways limesema limefuta safari zake zote za ndege hadi itakapofika saa kumi na moja jioni.

Kwa mujibu wa wataalam wa hali ya hewa hali kama hii ya kuanguka theluji nzito haijawahi kulikumba jiji la London kwa miaka 18 iliyopita.



Source: BBC

Prisons yanyukwa 2-0

WATANZANIA wana raha robo tu katika michuano inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika baada ya Yanga kuibuka timu pekee katika michezo ya mwanzo hatua ya awali, kwa kuitandika Etoile d’Or ya Comoro mabao 8-1.

Katika hali ya huzuni, timu nyingine tatu zimejikuta zikipata matokeo ya vipigo, hali inayoleta huzuni, kwani katika timu nne, ni Yanga inayoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika iliyoanza vizuri, tena kwa kishindo.

Lakini wawakilishi wengine katika michuano hiyo, Miembeni kutoka Zanzibar ilijikuta ikilambwa mabao 2-0 na Monomotapa ya Zimbabwe katika mchezo uliofanyika mjini Harare.

Katika michuano ya kuwania Kombe la Shirikisho (CAF), Tanzania Prisons ilibanjuliwa nyumbani jana na Khalij Sert ya Libya katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kipigo hicho kimekuja siku moja baada ya wawakilishi wengine kwenye michuano hiyo, Mundu ya Zanzibar kupigwa mabao 6-0 na Red Arrows ya Zambia, katika mchezo uliofanyika mjini Lusaka juzi.

Katika mchezo jana Tanzania Prisons walianza kuwa wanyonge mapema baada ya winga machachari wa Khalij, Abdullah Shaiji kupiga bao la kuongoza.

Nyota huyo, aliyeonekana kuwa nyota wa mchezo alifunga bao hilo katika dakika ya pili, baada ya kuwatoka mabeki wa Prisons na kupiga shuti na kipa wa timu hiyo, Exevery Mapunda, kuutema na kuumalizia tena kwa kisigino.

Prisons ambayo licha ya kufungwa ilitandaza soka safi katika kipindi cha pili cha mchezo huo na wachezaji wakongwe wa timu hiyo Yona Ndabila na Henry kukosa nafasi nyingi ambazo kama wangezitumia vyema, wangefunga.

Khalij ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao moja. Wakati timu zinaingia kipindi cha pili, mabeki wa Prisons walipata kibarua kigumu baada ya winga wa kushoto Masuud Ghinai kuwachosha, kutokana na kupiga chenga huku akiwa anakimbia.

Katika dakika ya 62, mshambuliaji wa kutegemewa wa Khalij, Saadulah Wafidia aliwanyanyua mashabiki na wapenzi wa timu hiyo ambao ni raia wa Libya waliojitokeza kuishangilia, baada ya kufunga bao la pili, alipopokea krosi safi kutoka kwa Dibati Musa.

Hadi kipenga cha mwisho cha Alfred Ndinya kinapulizwa, matokeo ya mchezo huo yalikuwa ni 2-0, kwa matokeo hayo Prisons itakuwa na kibarua kigumu cha kufanya vizuri katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Libya wiki mbili zijazo, kama ilivyo kwa timu nyingine za Tanzania, isipokuwa Yanga.

Akizungumzia mchezo huo, Kocha Mkuu wa Prisons, James Nestory, alisema papara za washambuliaji wake zimechangia kwa kiasi kikubwa kwa kuwachosha mabeki na viungo wa timu hiyo.


Sunday, February 1, 2009

Rais Mpya achaguliwa Somalia

Sheikh Sharif Ahmed , Rais mpya wa Somalia

Kiongozi anayefuata msimamo wa wastani wa WaIslamu, Sheikh Sharif Ahmed amechaguliwa kuwa rais mpya wa Somalia, baada ya kura ya siri ya wabunge wa Somalia.

Bwana Ahmed alishinda kwa kura za kutosha katika duru ya pili ya upigaji kura, baada ya mshindani mwenzake mmoja, Waziri Mkuu Nur Hassan Hussein kujitoa katika mashindano.

Bwana Ahmed amechaguliwa na bunge baada ya Rais Abdullahi Yusuf Ahmed kujiuzulu.

Wabunge walikutana Djibouti kwa vile hakuna utulivu Somalia, ambako wapiganaji Waislamu wanadhibiti sehemu kubwa ya nchi.

Bwana Ahmed alikuwa kiongozi wa upinzani ambao ukishutumiwa kuwa na mshikamano na Al Qaeda. Mwandishi wa BBC katika eneo hilo, Peter Greste, anasema Bwana Ahmed alishinda uchaguzi, kwa sababu anaonekana anaweza kushirikiana na pande mbili tofauti za wababe wa kivita, ambao hadi sasa wamekuwa wakiidhibiti serikali na wapiganaji wa Al-Shabab.

Mapema juma hili, wanachama wapya 149 kutoka upande wa upinzani wa Muungano wa Kuikomboa tena Somalia, ambao wanaongozwa na Bwana Ahmed, waliapishwa na kuwa wabunge.

Lakini Al-Shabab inasema kuwa haitoitambua serikali mpya; serikali ambayo inatarajiwa kuhama kutoka Djibouti hadi mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, katika siku chache zijazo.

Lakini Mogadishu inakabiliwa na fujo, na hakuna askari wa kutosha wa kuweka amani kutoka Umoja wa Afrika, kuweza kuwalinda wabunge. Inafikiriwa kuwa baadhi yao watabaki Djibouti na wengine watakwenda Kenya.

Wapiganaji wa Al-Shabab wanadhibiti mji wa Baidoa, ambako bunge zamani likikutana, pamoja na maeneo kadha ya kati na kusini mwa Somalia.


Source: BBC

Yanga yawachanachana Wacomoro

Yanga jana iliingia raundi ya pili ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika ambako itakutana na mabingwa watetezi National Al Ahly ya Misri baada ya kuichabanga Etoile d`Or Mirontsy ya Comoro kwa magoli 8-1 katika mchezo wa kwanza wa raundi ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa, Boniface Ambani akiona nyavu mara nne.

Yanga ilipata bao la kwanza katika dakika ya pili lililofungwa na Ambani kwa shuti kali lililomshinda mlinda mlango Maudese Mohamed.

Lakini katika mchezo ambao mshindi baada ya mechi ya marudiano atakumbana na bingwa mara sita wa Afrika Al Ahly, d'Or Mirontsy ilisawazisha katika dakika ya 20 kupitia kwa Aboubakar Alisoul aliyesindikizwa na walinzi wa Yanga na kosa la Juma Kaseja kutoka langoni mapema.

Itakuwa ni ajabu kama Yanga sasa itatolewa baada ya ushindi huo mkubwa licha ya ukweli kuwa itakabiliwa na tatizo la dharau pindi itakapokuwa ugenini wiki mbili zijazo.

Jerson Tegete aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Benard Mwalala alipachika bao la pili kwa shuti la nguvu katika dakika ya 54 baada ya kuwahi mpira uliopigwa na Ambani.

Dakika 16 baadaye Ambani aliongeza bao la tatu kwa penalti iliyotolewa na mwamuzi kutoka Uganda baada ya Mrisho Ngassa kufanyiwa madhambi na mmoja wa walinzi wa Etoile.

Mlinzi Wisdom Ndlove alipachika bao la nne kwa kichwa baada ya kuwahi mpira wa kona uliopigwa na Abdi Kassim katika dakika ya 74, na dakika mbili baadaye Tegete tena alipachika bao la tano baada ya kupokea pasi murua ya Vicent Barnabas aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Kigi Makassy.

Ambani ambaye ni kinara wa magoli katika ligi kuu akiwa amefunga magoli 13 hadi sasa alipachika bao la sita baada ya kupata pasi kutoka kwa Ngassa katika dakika ya 79, na dakika mbili baadaye Ngassa aliongeza bao la saba kwa shuti na Ambani alifunga kitabu cha magoli katika dakika ya 85 kwa kufunga bao la nane.

Kocha wa Yanga Dusan Kondic aliwapongeza wachezaji wake kwa kujua majukumu yao hasa katika kipindi cha pili na kusema pia hatadharau mchezo wa marudiano.

Naye kocha wa Etoile, Nasurdine Maanrouf alisema timu yake haina uzoefu katika michuano ya kimataifa na hii ni mara yao ya kwanza kushiriki.

Timu zilikuwa:
Yanga: Juma Kaseja, Shadrack Nsajigwa, Amir Maftaha, Nadir Haroub `Canavaro`, Wisdom Ndlove, Geofrey Bonny (Nurdin Bakari dk.44), Mrisho Ngassa, Abdi Kassim `Babi`, Boniface Ambani, Benard Mwalala (Jerson Tegete dk.46) na Kigi Makassy (Vicent Barnabas dk.55).

Katika mchezo wa raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho, Mundu ilifungwa mabao 6-0 na Red Arrows ya Zambia katika pambano lililofanyika mjini Lusaka jana Jumamosi, habari kutoka Zanzibar zilisema jana.

Wawakilishi wa Zanzibar katika michuano kama ya Yanga, Miembeni itacheza leo na Monomotapa ya Zimbabwe ugenini.




Source: Lete Raha